Hugh Hefner, mwanzilishi wa jarida la kimataifa la watu wazima - Playboy, amefariki akiwa na umri wa miaka 91.
Playboy Enterprises Inc imesema alifariki kwa amani nyumbani .
Hefner alianza kuchapisha jarida hilo jikoni nyumbani mwake mnamo 1953. Likawa jarida linalo uzika zaidi la wanaume duniani.
Cooper Hefner, mwanawe amesema "atakumbukwa kwa ukubwa na wengi".
Alimtaja babake kama "Mojawapo ya watu wa kwanza kujitosa katika uandishi na aliishi maisha ya aina yake na yenye utofuati," na amemuita mtu anayetetea uhuru wa kuzungumza, haki za kiraia na uhuru wa kijinsia.
No comments:
Post a Comment