Wakati
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji anapanda tena Mahakama ya Kisutu
kujibu kesi ya tuhuma za madawa ya kulevya, wanasheria wake wamesilisha
hati ya maombi kutaka apandishwe kizimbani kwa kesi ya uhamiaji.
Taarifa
zinaeleza, wanasheria wa Manji wamewasilisha hati hiyo mahakamani
wakitaka apandishwe mahakamani kwa kesi ya uhamiaji ambao wanamtuhumu
kuingia nchini kinyume na sheria.
Manji amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan lakini chini ya ulinzi wa Maofisa wa Uhamiaji pamoja Jeshi la Polisi.
Hata
hivyo kwa zaidi ya wiki tatu sasa, hajawahi kupandishwa kizimbani. Hali
iliyosababisha wanasheria wake kuwasilisha hati hiyo ya maombi.
No comments:
Post a Comment