Monday, February 13, 2017

MAN U NDIO TIMU YENYE POINTS NYINGI ENGLAND KUANZIA MWAKA 1992


Kikosi cha Jose Mourinho kimeonekana kuongeza wimbi la ushindi baada ya kuipiga Watford goli 2 kwa 0.Japokuwa United walishinda mchezo huo hawakufanikiwa kuondoka katika nafasi yao ya 6 baada ya Liverpool nao kushinda na kuwarudisha katika nafasi yao hiyo.

Ushindi wa Manchester United umewafanya waweke rekodi moja mpya katika ligi ya Uingereza.United wamekuwa timu ya kwanza kukusanya pointi 2000 katika ligi hiyo.Pointi ambazo ni nyingi zaidi kuwahi kufikiwa toka kuanzishwa kwa mashindano hayo.

United katika msimamo wa ligi kuu Uingereza safari hii wamepitwa na Chelsea pointi 11.Lakini United wameipita Chelsea pointi 244 kwa ujumla wa pointi toka ligi hiyo ianzishwe.Alama hizo wamezipata baada ya kushinda jumla ya michezo 599 na kwenda sare michezo 203 waliyocheza kuanzia mwaka 1992.

Si hivyo tu bali United pia ndio timu pekee ambayo ina wastani wa pointi 2 katika kila mechi.Huku Arsenal wakiwakaribia United kwa kuwa na wastani wa 1.89 na Manchester City wakiwa na wastani wa 1.51.

No comments:

Post a Comment