Ametoa
agizo hilo leo mchana (Jumatatu, Februari 13, 2017) katika kikao baina
ya Kamishna huyo mpya na Maafisa Magereza wa Mikoa yote na maafisa
wanaoshughulikia kilimo na viwanda alichokiitisha ofisini kwake mjini
Dodoma.
“Magereza
yetu mengi yako kwenye maeneo ambayo hayajapimwa. Baadhi ya maeneo kuna
migogoro kwa sababu wananchi wamejenga karibu kabisa na maeneo ya
Magereza. Lazima tupime maeneo yote na kuyawekea alama mipakani ili
kubainisha maeneo yetu,” amesisitiza.
Mbali
ya maeneo ya Magereza, Waziri Mkuu amesema, jeshi hilo lina mashamba
makubwa ambayo pia hayajapimwa hali ambayo amesema imechangia baadhi ya
wananchi kulima ndani ya maeneo ya jeshi hilo.
“Natambua
kuwa jeshi hili lina mashamba makubwa lakini nayo pia hayajapimwa. Kila
RPO ni mjumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wake, tumieni
wapima ardhi kutoka kwenye Halmashauri zenu na mhakikishe kuwa maeneo
hayo yanapatiwa hati,” amesema.
No comments:
Post a Comment