Pages

Wednesday, April 11, 2018

TPA YALETA MKANDARASI KUTOKA KOREA KUSINI KUJENGA MELI

Na James Timber, Mwanza
Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), jijini Mwanza imethibitisha Kampuni ya Korea Kusini  kuchukua Kandarasi ya ujenzi wa Meli kubwa  katika ziwa Victoria  lengo likiwa ni  kuboresha huduma ya bandari.

Akizungumza katika uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 13 ya Usimamizi wa Bandari, Mgeni Rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella alisema mazingira ya Bandari inazidi kuboreka  kutokana na Mji wa Mwanza kuwa Kitovu cha Maziwa Makuu Afrika Mashariki.

"Sisi mikakati yetu kupitia Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Dk. John Magufuli ni kuhakikisha wananchi wanapata fursa za ajira na biashara ambapo pato litaongezeka katika Halmashauri husika na Serikali Kuu," alisema Mongella.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Bandari mkoani hapa Daniel Sira alisema kuwa bandari hiyo,  lengo lake ni kuhudumia kiasi cha mizigo tani milioni moja na abiria milioni moja kwa kipindi cha  mwaka mmoja.

Sira alieleza kuwa  mamlaka hiyo  ina bandari mbili za nchi kavu, Bandari ya fera ambayo inatarajia kujengwa hivi karibuni na Isaka iliyoko kahama shinyanga.

Meneja huyo alisema wamekuwa karibu na jamii kwa kutoa huduma mbalimbali mashuleni na hosptalini ndani na mikoa jirani ya Kanda ya Ziwa.

No comments:

Post a Comment